July 7, 2014



Kamati ya usajili ya Simba chini ya Zacharia Hans Poppe imeonyesha imepania kweli kuboresha kikosi baada ya kumalizana kwa asilimia 95 na mshambuliaji hatari kutoka Kenya.
Modo Kiongera mwembamba, mrefu mfano wa Emmanuel Adebayor, msimu uliopita alikipiga Kenya Commecial Bank (KCB), ndiye mshambuliaji anayekuja nchini kusaidiana na Amissi Tambwe wa Burundi ‘kuchana’ nyavu za timu pinzani.
AKIWA NA LOGARUSIC

Kiongera ni kati ya wachezaji walio katika kikosi cha timu ya taifa ya Kenya, Harambee Stars na Kocha Adel Amrouche amezungumza na Championi JUmatatu na kusema Simba wakimnasa, watakuwa wamekula Bingo.

“Ni mmoja wachezaji ambao nimekuwa nikiwaita kwenye kiksoi changu, kama Simba wakimpata ni mmoja wa wachezaji bora,” alisema Amrouche raia wa Ubelgiji.
Taarifa za uhakika zinaeleza mchezaji huyo mrefu, mwenye sifa ya mashuti makali, anatarajia kutua nchini ndani ya siku mbili tayari kusaini mkataba wa kuichezea Simba.
AKIWA NA MUSOTI

“Kila kitu kinakwenda vizuri na kamati ya usajili chini ya Hans Poppe inafanya mambo yake kwa umakini mkubwa, hivyo Mkenya anakuja kuungana na Simba,” kilieleza chanzo.

“Mazungumzo yamekwenda vizuri, baada ya Kiongera kutua Dar nafikiri litakuwa ni suala la kumalizia tu, maana mambo yaliyobaki ni mdogo sana.”

Kiongera alikuwa mchezaji bora wa Ligi Kuu Kenya mwaka 2012 wakati akikipiga Gor Mahia kwa mkopo, mwaka huo ndiyo Kocha Zdravko Logarusic akabeba tuzo ya kocha bora nchini Kenya.

Taarifa zinaeleza, Logarusic ndiye aliyembeba Kiongera kutoka KCB kwa mkopo hadi Gor Mahia na baada ya hapo, wakaanza kukamua pamoja hadi kufikia kubeba ngao ya hisani na baadaye wakashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho.
Pamoja na Loga, mwingine aliyewahi kufanya kazi na Kiongera ni Donald Musoti na kipa Ivo Mapunda, sasa wanakutana tena Simba.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic