July 7, 2014


MKWASA NA PLUIJM WAKIWA NA MMOJA WA WACHEZAJI WALIO KATIKA KIKOSI CHAO

Makocha wa zamani wa Yanga, Hans van der Pluijm na msaidizi wake, wameanza kazi ya kuwanoa wachezaji kutoka mataifa tofauti manne.
Wachezaji hao wa kikosi cha Al Shaolah kinachoshiriki Ligi Kuu ya Saudi Arabia, wanatokea katika nchi hiyo mwenyeji, Jordan na mataifa mawili ya Afrika Ghana na Mali.
Akizungumza na Championi Jumatatu kutoka nchini humo, Pluijm alisema kadiri siku zinavyosonga mbele wamekuwa wakizoea mazingira.
“Kama nilivyowahi kuwaeleza awali, hali ya hewa ya joto kali ilikuwa inatusumbua, lakini sasa tumezoea,” alisema Pluijm raia wa Uholanzi.
“Lakini sasa mambo ni mazuri na mazoezi yetu yanakwenda vizuri sana. Tunaendelea vizuri kwa asilimia kubwa na tunachosubiri ni kuanza kwa msimu.”
Pluijm ndiye aliyeushawishi uongozi wa Al Shaolah kumchukua Mkwasa ambaye walifanya kazi kwa ushirikiano mzuri wakiwa Yanga.
SOURCE: CHAMPIONI

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic