July 22, 2014




Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic amesema Ligi Kuu Bara msimu ujao haitakuwa lahisi au lelemama, lakini mwisho Simba ndiyo itafanya vizuri.
Loga amesema ana uhakika kikosi chake kitafanya vizuri kama wachezaji wataendelea kuzingatia mazoezi na uongozi kuwapatia kila wanachotaka.
“Ili tiu ifanye vizuri kuna mambo mengi sana yanatakiwa kwenda sawa.
“Wachezaji lazima wawe makini na waelewe tunachokifanya ni nini kwa faida yao nay a timu.
“Pia wajue tunataka ushindi na mafanikio yatapatikana kwa kila mmoja kuwa na malengo na kufanya kazi yake kwa asilimia mia.
“Kwa upande wa uongozi, utekeleze kinachotakiwa kutoka kwa benchi la ufundi na mahitaji muhimu ya wachezaji,” alisema Logan a kuongeza.
“Naamini ligi itakuwa ngumu sana, lakini mwisho tutashinda hasa kama tutakwenda kwa mtiririko huo.”
Simba inaendelea na mazoezi yake ufukweni, pia kwenye Uwanja wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic