July 22, 2014




Pamoja na kuamua kumuacha kwa madai alitaka fedha nyingi, sasa Simba iko katika hatua za mwisho kumnasa mshambuliaji Mkenya, Modo Kiongera.
Mazungumzo kati ya Simba na Mkenya huyo aliyekuwa akikipiga KCB yako katika hatua nzuri.
Habari za uhakika kutoka ndani ya Simba, zimeeleza, Kocha Zdravko Logarusic amesisitiza kumpata mshambuliaji huyo.
Kiongera aliwahi kufanya kazi na Loga wakiwa Gor Mahia baada ya kocha huyo kutoka Croatia kumtwaa kwa mkopo kutoka KCB.
Simba ilianza harakati za kumnasa, lakini ikaelezwa bei yake ilipanda baada ya mmoja wa viongozi kuwavuruga wenzake.
Kamati ya usajili ikaamua kuachana naye lakini msisitizo wa Loga umefanya warudi kuendelea na mazungumzo naye na yako katika hatua za mwisho.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic