Hatimaye Luis Suarez ameichezea Barcelona kwa mara ya kwanza katika
mechi ya kirafiki dhidi ya FC Leon.
Barcelona ilishinda kwa mabao 6-0 kwenye Uwanja wa Cam Nou huku Lionel
Messi na Neymar aliyekuwa amjeruhi wakitikisa nyavu.
Burudani kubwa ilikuwa ni Suarez aliyeingia baadaye.
Alishangiliwa kwa nguvu na mashabiki na mshambuliaji huyo wa zamani wa
Liverpool akaingia na kuonyesha mbwembwe.
Hata hivyo atalazimika kurudi benchi wakati La Liga inaanza wikiendi
hii.
Atakuwa nje hadi Oktoba 26 kuitumikia adhabu yake ya Fifa kutokana na
kumng’ata beki Giorgio Chiellini wa Italia wakati wa Kombe la Dunia.
‘Usamjo’ umetumika kuipoza adhabu hiyo na sasa Suarez anaruhusiwa
kuendelea na mazoezi na Barcelona na pia kucheza mechi za kirafiki.
0 COMMENTS:
Post a Comment