Mshambuliaji wa Besiktas ya Uturuki, Demba Ba na wenzake, wametengewa
dau la pauni 850,000 ili waizamishe Arsenal ya Arsene Wenger.
Iwapo watashinda mechi hiyo ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kuwania kucheza
hatua ya makundi, watakuwa wamejiweka safi kabla ya mechi ya marudiano
itakayopigwa jijini London.
ARSENAL WAKIWA NJIANI KWENDA UTURUKI. |
Tayari Arsenal wametua nchini Uturuki kwa ajili ya pambano hilo la leo
na Ba aliyekuwa akikipiga Chelsea na wenzake wanajua kuhusiana na suala hilo.
0 COMMENTS:
Post a Comment