Ndanda inayodhaminiwa na kampuni ya Bin Slum Tyres Ltd inayotengeneza
bidhaa mbalimbali za matairi kama Double Star, Vee Rubber na rim za Topu,
imejigamba kuwa itafanya maajabu kwenye msimu ujao.
“Tunalenga kufanya vizuri, tunajua ushindani mkubwa katika ligi. Lakini
tutapambana na kuwashanga wengi.
“Wengi wanaweza wakatudharau lakini watashangaa,” alisema Ngawina
akionyesha kujiamini.
Ndanda baada ya kupata udhamini wa Bin Slum, ni dalili kuwa italeta
ushindani mkubwa.
Kikosi cha Ndanda kinaendelea kujifua kwenye Uwanja wa Chuo Kikuu cha Ardhi jijini Dar es Salaam.
Ligi Kuu Bara imepangwa kuanza Septemba 20 na Ndanda ni kati ya timu tatu zilizopanda. Nyingine ni Stand United ya Shinyanga na Polisi Moro.
0 COMMENTS:
Post a Comment