MTIBWA SUGAR YA MSIMU ULIOPITA |
Timu za Mtibwa Sugar na Polisi Morogoro
zinazojiandaa na Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) zitacheza Jumamosi (Agosti 23 mwaka
huu) mechi ya majaribio ya mfumo wa tiketi za elektroniki.
Mechi hiyo itafanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri
mjini Morogoro kuanzia saa 10 jioni wakati kiingilio kitakuwa sh. 1,000.
Tiketi za mechi hiyo zitaanza kuuzwa kesho
(Agosti 20 mwaka huu) kupitia mtandao wa M-Pesa, CRDB Simbanking na maduka 30
ya Fahari Huduma yaliyopo katika wilaya zote za Mkoa wa Morogoro, wengi wao
wakiwa Morogoro Mjini.
Washabiki 100 wa kwanza kuingia uwanjani wapata
jezi za timu za Mtibwa Sugar na Polisi.
Tayari mechi ya majaribio ya tiketi za
elektroniki imeshafanyika kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya
ambapo timu za Tanzania Prisons na Mbeya City zilipambana na kutoka sare.
Mechi nyingine za majaribio ya tiketi za
elektroniki zitachezwa Agosti 30 mwaka huu. Uwanja wa Mkwakwani jijini utakuwa
na mechi kati ya Coastal Union na Mgambo Shooting wakati katika Uwanja wa
Kaitaba mjini Bukoba ni Kagera Sugar dhidi ya mabingwa wa Mkoa wa Kagera,
Eleven Stars.
Septemba 6 mwaka huu katika Uwanja wa Taifa kutakuwa na mechi
kati ya Simba na Mtibwa Sugar. Mechi nyingine ni ya Ngao ya Jamii kati ya Azam
na Yanga itakayofanyika Septemba 13 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
0 COMMENTS:
Post a Comment