August 15, 2014


BANDA WAKATI AKIWA COASTAL...


Wakati Coastal Union wakiendelea kumlilia beki Abdi Banda, mchezaji huyo ambaye amesaini mkataba wa kuichezea Simba, amepewa nyumba ya kuishi.


Hatua hiyo imekuja siku chache tangu mshambuliaji wa Simba, Mrundi Pierre Kwizera, kupewa nyumba ya kuishi pia maeneo ya Kunduchi.

Banda amepewa jumba eneo la Mikocheni huku ikikumbukwa kuwa enzi za utawala wa Mwenyekiti Ismail Aden Rage mchezaji aliyeishi sehemu za gharama kubwa alikuwa ni straika Amissi Tambwe ambaye alipangishiwa mitaa ya Sinza.

“Mimi si mwenyeji wa Dar, viongozi wameniambia kuwa tayari wamenitafutia nyumba Mikocheni na ndani ya wiki hii ninaweza kuhamia,” alisema Banda.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic