August 15, 2014



Kocha Mkuu wa Yanga, Marcio Maximo amesema nia kubwa ya kwenda kuweka kambi Pemba ni kufuata vitu muhimu vitatu.


Maximo amesema kuwa kwa siku chache alizokaa na kikosi amefurahishwa na mabadiliko ya wachezaji wake na kusema kuwa mambo hayo matatu yakikamilika, basi kikosi chake kitakuwa tayari kwa msimu mpya.

Kocha huyo raia wa Brazil ametaja mambo hayo kama ifuatavyo: “Mbinu, nitaanza na suala hili kwanza kwa kuwa nitakuwa na wachezaji wote.

“Nitatengeneza programu maalumu kwa kusaidiana na makocha wenzangu jinsi ya kuwatumia mabeki, viungo na washambuliaji.

“Jambo la pili ni ufundi, hili nalo linatakiwa kukamilika kabla ya mechi ya Ngao ya Hisani (dhidi ya Azam).

“Tatu ni nguvu, ili kikosi kiimarike basi lazima wachezaji wawe na nguvu na stamina. Hayo ndiyo mambo matatu makubwa lakini kutakuwa na vitu vingine nikiwa visiwani huko.”

Lakini pia kulikuwa kuna taarifa za kuwa wachezaji wa Yanga hawajalipwa mishahara yao.

Kiongozi mwingine wa Yanga aliliambia gazeti hili kuwa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), ambao ni wadhamini wa klabu hiyo wamechelewesha kuipa klabu hiyo fedha za udhamini na ndiyo maana mishahara imechelewa pia.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic