Mwanariadha nyota wa Jamaica, Usain Bolt ameendelea kutesa katika mbio
za mita 100 kushinda katika michuano ya Copa Cabana jijini Rio de Janeiro,
Brazil, jana.
Bolt alishinda kwa sekunde 10.6 mbele ya wanariadha wengine nyota kama Mark
Lewis Francis, American Wallace Spearmon na Brazilian Jefferson Liberato
Lucindo.
Bolt, 27, alishangiliwa kwa nguvu na watu waliojazana kwenye ufukwe huo
wakati akiondoka.
Ndiye mwanariadha anayeshikilia rekodi ya juu katika mita 100 ya sekunde
9.58.
|
0 COMMENTS:
Post a Comment