August 16, 2014



Kocha Mkuu wa Yanga, Marcio Maximo amejikuta akitumbukia katika lindi la mawazo baada ya kuwakosa mazoezini nyota wake, Andrey Coutinho na Kelvin Yondani.
Wachezaji hao kwa pamojana jana walishindwa kufanya mazoezi na wenzao ya kujiandaa na msimu ujao wa Ligi Kuu Bara kutokana na kusumbuliwa na maradhi mbalimbali.
Hali hiyo imemfanya Maximo aonekane kuwa ni mwenye mawazo mengi kutokana na kutojua siku ambayo wachezaji hao ambao ni kati ya nyota wake wa kutumainiwa watarudi uwanjani kuendelea na kazi yao.
Daktari wa Yanga, Juma Sufiani amesema wachezaji hao ni wagonjwa na ndiyo maana katika mazoezi ya jana hawakuweza kuonekana uwanjani.
Alisema Coutinho ambaye amejiunga na klabu hiyo hivi karibuni akitokea nchini Brazil, anasumbuliwa na maumivu ya mgongo wakati Yondani anasumbuliwa na Malaria.
“Hata hivyo kwa sasa wanendelea vizuri baada ya kupatiwa matibabu hivyo nimatuini yetu kuwa watarudi uwanjani hivi karibuni kabla ya safari yetu ya Kisiwani Pemba,” alisema Sufiani.
Kikosi hicho cha Yanga kinatarajia kuonda Dar es Salaam, Jumatatu hii na kwenda Pemba kwa ajili ya kupiga kambi ya siku 10 ya kujiandaa na msimu ujao wa Ligi Kuu Bara unaotarajia kuanza kutimua vumbi Septemba 20 mwaka huu.
SOURCE: CHAMPIONI JUMAMOSI

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic