MUSOTI (KULIA KWA UHURU) AKIMSIKILIZA KWA UMAKINI MKUBWA KOCHA PHIRI. |
Beki wa kati wa Simba,
Mkenya Donald Musoti ametamka wazi kwamba kocha wake mpya wa sasa, Mzambia
Patrick Phiri yupo ‘soft’, kitu ambacho alikiri kuwa ni tofauti sana na kocha
wake wa zamani wa Zdravko Logarusic raia wa Croatia.
Musoti alifafanua kauli
yake hiyo ya soft kwamba ni kocha ambaye mpole na si mkali wakati wa utendaji
wake wa kazi katika kuhakikisha mchezaji anayaelewa mafuno yake kitu ambacho
kimemfanya amkubali zaidi kocha huyo tofauti na Loga aliyekuwa anatumia ukali
zaidi katik kuelekeza.
“Unajua huyu Phiri yupo
soft sana lakini yule Loga alikuwa ‘hard’ mno katika ufundiahji wake, kila
kocha ana staili yake na ujanja wake wakati wa ufundishaji, lakini nikwambie tu
ukweli kamba nimefurahishwa sana na ufundishaji wa Phiri.
“Loga niliwahi kuwa nae Gor
Mahia namfahamu lakini Phiri ndio kwanza nimekutana nae Simba lakini nimekuwa
nikimuona na kupata taarifa zake kutoka kwenye wachezaji mbalimbali aliowahi
kuwafundisha hapa Afrika Mashariki, ni kocha mzuri kwa kweli,” alisema Musoti.
0 COMMENTS:
Post a Comment