August 15, 2014



Familia za viongozi wa benchi la ufundi na madereva wa timu ya taifa, Taifa Stars, wamelilalamikia Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) juu ya kutolipwa fedha zao wanazotakiwa kulipwa kutokana na majukumu yao.


Taarifa kutoka ndani ya benchi la ufundi la Stars zilizofika mezani katika gazeti hili ni kuwa hakuna kiongozi aliyelipwa fedha za posho na malimbikizo mengine tangu timu hiyo ilipoanza ushiriki wa kuwania kufuzu Afcon 2015, mpaka hatua ya kutolewa.

Mhusika mmoja kutoka kwenye benchi hilo amesema kuwa uwezekano wa wao kulipwa haki zao unaonekana kuwa mdogo kwa kuwa Rais wa TFF, Jamal Malinzi hajaonyesha mwelekeo wowote juu yao.

“Wao (TFF) waliwalipa wachezaji tu, lakini benchi la ufundi na madereva wanadai hadi hivi sasa na haijulikani watatulipwa lini. Mwambieni rais anatuua kwa njaa.

“Tumevumilia sana, lakini hivi sasa uvumilivu tunaona umeanza kutushinda, kwa sababu familia zetu hazituelewi,” alisema mtoa taarifa huyo akionyesha kuwa na uchungu.

Juhudi za kumpata Malinzi kulizungumzia suala hilo, zilikuwa ngumu kwani pamoja na kupokea simu mara ya kwanza na kuulizwa swali, alisema:
 “Naomba unipigie baada ya dakika 20, kuna kazi ninamalizia.” 

Lakini baada ya hapo, simu yake ilikuwa ikiita bila ya kupokelewa hata kidogo.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic