August 15, 2014

MGOSI WAKATI AKIWA SIMBA


Mshambuliaji mkongwe wa Mtibwa Sugar, Mussa Hassan Mgosi na kiungo mkabaji wa timu hiyo, Vincent Barnabas, mapema wiki hii walitoa kali baada ya kugombea vitumbua mara baada ya mazoezi katika Uwanja wa Bora, Kijitonyama jijini Dar es Salaam.


Wachezaji hao waliokuwa wamekaa pembeni mwa uwanja huo, walianza kuvishambulia vitumbua hivyo vilivyokuwa kwenye gari aina ya Noah huku wakivisifia kuwa vimepikwa vizuri na kumsifia mpishi wa msosi huo.

“Kiukweli vitumbua ni vitamu sana, usipoangalia unaweza kujikuta unakula mpaka ukavimbiwa, huyu mama aliyepika kavipatia sana,” alisikika Barnabas akimwambia Mgosi huku wachezaji wengine nao wakipaza sauti kuomba wasimaliziwe vitumbua hivyo.

Wakati huohuo, katika mazoezi ya timu hiyo, kocha msaidizi wa timu hiyo, Zuberi Katwila, aliwataka wachezaji kucheza kwa umakini mkubwa kwa kuwa hawajapata daktari.

“Timu bado haijapata daktari wa kudumu, nimewaambia wawe makini,” alisema.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic