August 9, 2014



Na Saleh Ally
HATA kama itaonekana ni kazi lahisi lakini wiki moja ijayo ndiyo itakuwa ngumu sana kwa Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic, kwa maana ya kufanya uamuzi wa kitaalamu zaidi.
Uongozi wa Simba umeamua ‘kujilipua’, umewaleta washambuliaji watatu kutoka nchi tatu na wote wanachezea timu za taifa, lakini anatakiwa mmoja tu.


Loga ndiye atakuwa na jukumu la mwisho la kuamua kuhusiana na washambuliaji hao watatu ambao ni Modo Kiongera ni raia wa, Ousimanou Manneh kutoka Gambia ambaye imeelezwa anakipiga nchini Senegal na Jerome Ramatlhakwane maarufu kama Rama raia wa Botswana anayekipiga TP Mazembe iliyomtoa kwa mkopo Don Bosco ya DR Congo.

Kwa maana ya takwimu, karibu wote wanaweza kuwa wachezaji wazuri wakatoa msaada kwa Simba ingawa lazima waonyeshe kwa vitendo.
Ukiangalia takwimu, Rama ndiye anaonekana ana uwezo mkubwa zaidi katika upachikaji mabao na changamoto ya mabadiliko ya soka la Botswana kupanda haraka, unaweza kushawishika kumpa nafasi ya kwanza kuwa anastahili.

Kiongera, bado ni kati ya wachezaji bora na wenye kiwango bora na anaichezea Harambee Stars kama mmoja wa washambuliaji wanaopewa nafasi ya pili baada wale wanaocheza nje ya Kenya.

Manneh si mshambuliaji mzoefu sana, huenda uwezo wake atakapofanya kazi mbele ya Loga kunaweza kukawa na majibu mazuri zaidi. Lakini suala la umri wa miaka 19, linaweza likawa linambeba.
Kwa kuangalia walivyo, unaweza kusema nafasi ya kwanza ni kwa Rama, pili Kiongera na Manneh abaki nafasi ya tatu.

Lakini kwa kuwaona kunaweza kukawa na jibu sahihi zaidi yupi atakuwa msaada kwa Simba, ingawa bado Loga anatakiwa kukubali kuwapa muda zaidi Rama na Manneh.
Kiongera na Loga wamewahi kufanya kazi pamoja wakiwa Gor Mahia.
Hivyo Rama na Manneh anatakiwa kuwaona na kutoa uamuzi ambao utakuwa sahihi na si ule wa hisia kama ulivyoanza kuhisiwa kwamba yeye anaamini Kiongera ni sahihi.
Ana haki ya kufikiri hivyo kwa kuwa anaijua kazi yake, lakini kuweka uwanja wazi awaone na Rama na Manneh, litakuwa jambo zuri na uamuzi wake wa mwisho utakuwa kwa manufaa ya Simba na hata usalama kwa kibarua chake.
Siku zote timu inakuwa ni mawazo ya wengi yanayoongozwa na wachache. Mtihani kwa Loga unaweza ukawa mgumu au lahisi kutokana na uwezo utakaoonyeshwa na washambuliaji wote.
Kama watakuwa wanatofautiana sana kiwango, kwake itakuwa lahisi kung’amua mambo mapema na kwa ulahisi zaidi.
Lakini viwango vyao vikiwa vinakaribiana, basi bila shaka kila kitu kitakuwa kigumu na umakini utalazimika kuongezeka.
Kwa uongozi wa Simba, pia unapaswa kumuamini Loga kutokana atakayemchagua kwa kuwa mwisho mbeba lawama ni kocha. Na isitokee kukawa kuna kiongozi anahitaji kufurahisha nafsi yake.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic