August 24, 2014




Mshambuliaji wa JS Kabylie, Albert Ebosse ameuwawa uwanjani wakati wa mechi ya Ligi Kuu nchini Algeria.
Ebosse raia wa Cameroon ameuwawa baada ya kupigwa na kitu kilichorushwa kutoka jukwaani wakati timu yake ikiivaa USM Alger.
Katika mechi hiyo iliyopigwa juzi, JS Kabylie iliishinda USM Alger kwa mabao 2-1, moja likiwa limefungwa na Ebosse mwenye umri wa miaka 24.
Ilionekana mashabiki wa USm Alger ambao wamekuwa wakielezwa kuwa na tabia za kibaguzi walirusha kitu ambacho kilimpiga kichwani akaanguka na kupoteza fahamu, baadaye maisha.
Mechi hiyo yenye upinzani mkali ilipigwa katika eneo la Tizi Ouzou nchini Algeria na tayari serikali ya nchi hiyo imesema imeanza uchunguzi wa jambo hilo.




0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic