Makocha wa kombaini za mikoa zitakazoshiriki Copa
Coca-Cola mwaka 2014 pamoja na waamuzi vijana wa michuano hiyo watashiriki kozi
ya ukocha na uamuzi itakayofanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Agosti 25 hadi
29 mwaka huu.
Kozi hiyo itafanyika jijini Dar es Salaam kuanzia
Agosti 25 hadi 29 mwaka huu ikiwa ni sehemu ya maandalizi michuano ya Copa
Coca-Cola ngazi ya Taifa itakayochezwa Septemba mwaka huu.
Makocha watakaoshiriki kozi hiyo na mikoa yao
kwenye mabano ni Ahmed Simba (Mwanza), Ally Kagire (Kagera), Aloyce Mayombo
(Pwani), Andrew Zoma (Tabora), Anthony Mwamlima (Mbeya), Athuman Kairo
(Morogoro), Bakari Ali (Kaskazini Pemba) na Charles Mayaya (Shinyanga).
Fidelis Kalinga (Iringa), Gabriel Gunda
(Singida), Hafidh Muhidin Mcha (Kusini Pemba), Hamis Mabo (Kigoma), John
William (Geita), Joseph Assey (Shinyanga), Joseph Haley (Manyara), Jumanne
Ntambi (Kilimanjaro), Leonard Jima (Ruvuma), Madenge Omari (Mara), Mohamed Muya
(Dodoma), Nicholas Kiondo (Ilala) na Nurdin Gogola (Temeke).
Osuri Kosuli (Simiyu), Peter Amas (Arusha),
Ramadhan Abdulrahman Ramadhan (Mjini Magharibi), Renatus Mayunga (Kinondoni),
Samwel Moja (Lindi), Seif Bakari (Katavi), Shaweji Nawanda (Mtwara), Sheha
Khamis Rashid (Kaskazini Unguja), Tigana Lukinjo (Njombe), Yusuf Ramadhan Hamis
(Kusini Unguja), Zahoro Mohamed (Tanga) na Zakaria Mgambwa (Rukwa).
Waamuzi vijana watakaoshiriki kozi hiyo chini ya Mkufunzi wa
FIFA, Felix Tangawarima wa Zimbabwe ni 33. Kwa upande wa ukocha Mkufunzi ni
Ulric Mathiott kutoka Shelisheli..
0 COMMENTS:
Post a Comment