Waamuzi wanaotarajia kuchezesha mechi za Ligi Kuu
ya Bara na Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu huu watafanya mtihani wa
utimamu wa mwili (physical fitness test) mwezi ujao.
Mtihani huo utahusisha waamuzi wa daraja la
kwanza (class one) wakiwemo pia wale wenye beji za Shirikisho la Kimataifa la
Mpira wa Miguu (Fifa).
Mbali ya mtihani huo unaotarajiwa kufanyika kabla
ya Septemba 10 mwaka huu, pia kutakuwa na semina kwa makamishna ambao
watasimamia mechi za VPL na FDL.
Hivyo waamuzi wote wanatakiwa kutumia muda uliobaki kufanya
maandalizi kwa ajili ya mtihani huo.
0 COMMENTS:
Post a Comment