August 13, 2014



Mshambuliaji Mganda, Hamisi Kiiza, ameanza rasmi mazoezi na klabu yake chini ya kocha mkuu wa timu hiyo, Mbrazil, Marcio Maximo ambaye anaangalia uwezo wa mchezaji huyo pamoja na wale wengine ambao wote walikuwa wakizitumikia timu zao za taifa.

 Wachezaji ambao walikuwa timu za taifa za nje ni pamoja na Emmanuel Okwi, Haruna Niyonzima na Hamis Kiiza na wale wa Tanzania   Kelvin Yondani, Mrisho Ngassa, Simon Msuva, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Oscar Joshua.
Straika huyo ameanza mazoezi rasmi klabuni hapo siku ya Jumatatu akitokea nchini kwao Uganda na kocha  wa timu hiyo anataka kupima uwezo wa mchezaji huyo na kama ataridhishwa, ataendelea naye.
Uongozi wa Yanga umemtaka kocha Maximo kuangalia uwezo wa Waganda hao wawili kati ya Kiiza na Okwi ili wajue nani wa kumuacha kwa jinsi alivyowaona kwa kuwa idadi ya wachezaji wa kigeni imezidi na kufikia 6 hadi sasa huku ikiwa imebaki nafasi moja pekee ya mchezaji mmoja wa nje kuendelea kuitumikia klabu hiyo ambapo ni lazima mmoja tu afungashiwe virago.

Aidha, straika huyo alikuwa akifanya mazoezi kwa bidii huku mara kadhaa akionekana kuwa makini na alichokuwa akielekezwa na kocha ikiwa ni pamoja na kuzungumza naye mambo kadhaa katika mazoezi hayo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic