August 16, 2014



Kocha mkuu wa timu ya Yanga Marcio Maximo ameweka msisitizo katika safu yake ya ulinzi baada ya kuwapa mazoezi maalum ya uokoaji wa mipira.


Maximo anaongoza mazoezi ya timu ya Yanga yanayo fanyika katika uwanja wa shule ya Loyola jijini Dar es Salaam.
Katika mazoezi hayo, kocha huyo alitoa zoezi maalum kwa mabeki la kuondoa mipira ya krosi itakayopigwa na wachezaji wa timu pinzani. Maximo alitaka kuhakikisha kila krosi itakayopigwa katika lango la Yanga, basi mabeki wa Yanga ndio wawe wa kwanza kuicheza.
Kwa zaidi ya dakika 25, Maximo alikua akiurusha mpira kuelekea golini huku akiwataka mabeki hao kuuondoa katika eneo la hatari kwa kuupiga kichwa. Zoezi hilo lilikomaliwa hadi alipoona kuwa mabeki wote wamelifanya kwa ufasaha na kwa jinsi atakavyo yeye.
Zoezi hilo liliwahusisha mabeki wa Yanga akiwemo nahodha Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Juma Abdul, Oscar Joshua, Said Juma, Rajab Zahir na Issa Ngao. 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic