Beki wa zamani wa Yanga, Abubakari Mtiro amefanikiwa
kusaini mkataba wa mwaka mmoja na klabu ya Kagera Sugar ili kujiunga na jahazi
hilo kukipiga katika Ligi Kuu Bara msimu ujao unaotarajiwa kuanza septemba 20,
mwaka huu.
Beki huyo aliyekuwa akiitumikia klabu ya
Ashanti United ameasaini katika klabu hiyo ya mkoani Kagera ambapo atakutana na
beki wa zamani wa yanga Ibrahim Job kujenga ukuta imara wa klabu hiyo.
Beki huyo
mwenye mwili uliojengeka kimazoezi alisema kuwa kwa sasa anamshukuru Mungu
kwani timu hiyo ina mipango mizuri ambapo mpaka sasa wanaendelea vema na
mazoezi kwa ajili ya kujiwinda na msimu ujao dhidi ya wapinzani wao.
“Nimesaini mkataba wa mwaka mmoja ambapo
nitaitumikia klabu hii kwa kutimiza wajibu wangu ili kuleta maendeleo yenye
sura mpya kwa kushirikiana na wenzangu katika suala zima la soka.
“Kwa msimu ujao Ligi Kuu Bara ninaamini
ushindi tutaupata kwa juhudi mbalimbali ambazo zinaendelea katika klabu yetu
huku tukijiandaa kucheza michezo kadhaa ya kirafiki kabla ya Ligi kuanza
kutimua vumbi,” alisema Mtiro.
0 COMMENTS:
Post a Comment