TANZANIA ELEVEN |
KIKOSI cha Tanzania Eleven kilicheza mechi
safi ya kirafiki dhidi ya wakongwe wa Real Madrid na kuishia kulala kwa mabao
3-1 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, juzi.
Pia walijitokeza kwa wingi kwa kuwa walitaka
kuwaona nyota kama Malota Soma, Mao Mkami, Clement Kahabuka, Abubakari Kombo,
Kali Ongala, Iddi Moshi, Madaraka Selemani, Nassor Mwinyi Bwanga, Mtwa Kihwelo,
John Mwansasu, Sabri Ramadhani ‘China’ na wengine wengi.
Mechi ilikuwa nzuri lakini hakuna ubishi kwamba Madrid walicheza vizuri
zaidi na kuonyesha kwamba wameishi katika maisha ya kufanya mambo yao katika
mpangilio mzuri zaidi.
Bado unaweza kusema, wakongwe wetu wa
Tanzania Eleven walijitahi na huenda bado wamo kisoka ingawa kisingizio
kinaweza kuwa timu hiyo haikuwa na muda wa kutosha wa mazoezi pamoja. Kikubwa
ambacho ninazungumzia leo ni mizengwe iliyokuwa imetawala kwenye kikosi hicho.
Mara baada ya kuteuliwa na hata kilipocheza.
Kilijaa mizengwe lukuki huku tayari kukiwa na watu wasiowataka wachezaji fulani
kuachwa kwa wachezaji ambao walionekana wangekuwa na msaada na wana uwezo wa
juu zaidi.
Unaweza kujiuliza kwa timu ile kwa nini
uwaache nje Malota Soma na Clement Kahabuka ambao wako fiti kuliko Emmanuel
Gabriel ambaye alilazimishwa kucheza akiwa anajulikana ana tatizo la goti?
Kwa nini wengine warudi uwanjani mara mbili,
mfano Kally na China ambao walitolewa na kuingia, halafu wengine wakabaki nje?
Jiulize kama kocha aliamua kuwatoa, vipi akawarudisha tena.
Je, waliokuwa nje wote wasingeweza kucheza
safu ya ushambuliaji kama Malota au Kahabuka halafu Kally narejea tena?
Nimejaribu kufuatilia mengi hadi kufikia kuandika hii.
Lakini utaona kuna watu walisema hivi,
wengine walijiita viongozi wakasema vile. Wako waliwasingizia makocha maneno
haya au yale. Makocha pia wanaweza kukuambia nafasi za kucheza zisingetosha.
Utaona Real Madrid walikuwa na watu 11
kwenye benchi wakati Tanzania Eleven ilikuwa na watu 16 ambayo ni timu
nyingine. Ndiyo maana nasisitiza, China na Kally hawakuwa na sababu ya kurejea
mara mbili na kocha angeona wako safi, hakuwa na sababu ya kuwatoa.
na ninaamini kuna watu watakuwa hawazungumzi
tena baada ya mechi hiyo kupita.
Hao ndiyo wakongwe, walichokifanya kwenye
mechi hiyo achana na kile cha uwanjani, lakini mizengwe ambayo huenda kwa mashabiki
ingekuwa si lahisi kuyajua, ndiyo majibu ya mpira wetu ulivyo.
Umejaza watu wasiopendana, watu wasiotaka
fulani aujulikane, kuonekana au kufanikiwa. Sasa mpira wenyewe utapiga vipi
hatua kwenda kwenye mafanikio wakati walio ndani yake hawataki watu wafanikiwe?
Wakongwe wameonyesha kuwa enzi zao pamoja ya
kuwa na sifa nzuri kama kujituma licha ya kwamba walilipwa kidogo. Lakini
wamethibitisha walikuwa na kasoro ya kutopendana na kutakiana mema, huenda
ndiyo maana Tanzania haikufanikiwa sana kisoka.
Tujiulize, tabia hizo mbaya ndiyo vijana
wetu wa sasa wamerithi kutoka kwa baba zao ndiyo maana mchezo wa soka umefunga
breki na sasa umekuwa ni ule wa hadithi nyingi tu?
Kuna jambo kubwa la kujifunza kupitia kikosi
hicho. Tuanzie uwanjani kwa tuliyoyaona kwa kuwa kama ni mazuri pia yapo.
Lakini niwasisitize vijana
wanaocheza au wanaojiandaa baadaye kuwa wachezaji nyota kwamba zengwe, chuki,
haliwezi kuusaidia mpira wa Tanzania, hilo msiige, waachieni hao wazee wenu
wazee nalo, waende nalo. Upendo na kutakiana kheri ni sehemu ya nguzo za
mafanikio.
0 COMMENTS:
Post a Comment