August 22, 2014



Kiungo mshambuliaji aliyetemwa Simba, Zahoro Pazi amesema kuwa kwa sasa inabidi achukue uamuzi mgumu maana ndiyo itakuwa njia sahihi kwake kupata haki yake, ambapo uamuzi huo ni kuishitaki klabu hiyo kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) baada ya kutopata barua au taarifa yoyote ya kumuacha kwenye usajili.


Pazi ni mtoto wa kipa wa zamani wa Simba ambaye sasa ni kocha wa makipa katika kikosi hicho kilichoweka kambi Zanzibar.

Pazi ni mmoja wa wachezaji waliotemwa na klabu hiyo wakiwa bado na mikataba pamoja na wenzake Ali Badru, Edward  Christopher na Betram Mwombeki na wengine ambao mikataba yao ilikuwa imemalizika ni Ramadhan Chombo ‘Redondo’, Salum Omar, Abuu Hashimu na Hassan Khatibu.

“Kwa sasa sina jinsi, nilichoamua ni kufuata sheria, napeleka barua yangu kwa TFF kwa sababu Simba wameshindwa kuwa waungwana kwa kushindwa kutimiza majukumu yao,” alisema Pazi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic