Kocha wa Simba SC, Mzambia, Patrick Phiri, amewapa masharti mapya wachezaji wake
ikiwemo kuwapiga marufuku kukaa chini muda wa mazoezi, hata kama wakiambiwa
wapumzike.
Hilo
limejiri hivi karibuni wakati Simba ilipokuwa ikiendelea na mazoezi kisiwani
Zanzibar kwenye Uwanja wa Chuo Kikuu cha Kiislamu, Chukwani ambapo Phiri
alikataza wachezaji waliokuwa pembeni wakipumzika wakisubiri ratiba nyingine,
kukaa chini wakiwa kwenye mchakato wa mazoezi.
Katika
mazoezi hayo, wachezaji wa Simba waligawiwa katika vikosi vitatu ambapo viwili
vilikuwa uwanjani, kile kingine ndipo wachezaji wake wakaamua kukaa chini
kuwasubiri wenzao.
Bila
kuchelewa, Phiri alipoliona tukio hilo, alilazimika kuwafuata wachezaji hao na
kuwaambia kuwa hawatakiwi kukaa chini wakati wakiwa kwenye programu ya mazoezi,
badala yake wanatakiwa kusimama hata kama wakiwa wanapumzika au wanakunywa
maji.
“Hamtakiwi
kukaa chini kama hivyo, kama ukiwa kwenye programu ya mazoezi ya kitimu kama
hivi unatakiwa kupumzika kwa kusimama na hata ukinywa maji hupaswi pia kukaa
chini, hili lisijirudie tena,” alisikika Phiri akiwaonya wachezaji wake hao.
0 COMMENTS:
Post a Comment