August 24, 2014




Hatimaye makocha Patrick Phiri wa Simba na Marcio Maximo wa Yanga, wamekutana hata kabla ya pambano la watani hao.
Wawili hao wamekutana leo kwenye Uwanja wa Amaan mjini hapa.
Yanga ilikuwa uwanjani hapa kuivaa Shangani na kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 na baadaye Simba ikawavaa Chipukizi.
Maximo kutoka Brazil alionyeshwa na Msemaji wa Yanga, Baraka Kizuguto kuwa Phiri raia wa Zambia alikuwa jukwaani.
Naye bila ya kuchelewa, mara moja akapanda juu na kumfuata Phiri na kupiga naye stori kwa dakika kadhaa huku wote wakionekana kuwa na furaha.
Makocha hao wawili, wamekutana kwa mara ya kwanza baada ya wote kurejea nchini.
Kawaida wangekutana Oktoba 12 kwenye mechi ya Ligi Kuu Bara dhidi ya watani hao.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic