Real Madrid imeshindwa kuutumia vizuri uwanja wake
wa nyumbani baada ya sare ya mabao 1-1 dhidi ya Atletico Madrid katika mechi ya
Super Cuo ya Hispania.
Real walifanikiwa kupata bao katika dakika ya 81 kupitia
James Rodríguez likiwa ni bao lake la kwanza akiwa na kikosi chake hicho kipya.
Lakini Atletico maarufu kama Rojiblancos
walifanikiwa kusawazisha dakika saba baadaye kupitia Raúl García aliyeuzungusha
mpira mitaa ya ‘far-post’.
Timu hizo mabingwa wa La Liga na wale wa Copa del
Rey sasa watakutana tena Ijumaa katika mechi hiyo ya marudiano.
0 COMMENTS:
Post a Comment