PHIRI AKIWA AMEMKUMBATIA UHURU, SIKU HIYO ALIKUWA AKITAMBULISHWA KWA WACHEZAJI WA SIMBA MARA BAADA YA KUSAINI MKATABA WA MWAKA MMOJA KUIFUNDISHA. |
Uongozi wa Simba umemuongezea mkataba wa mwaka
mmoja kiungo wake mshambuliaji, Uhuru Selemani.
Chanzo hicho kilisema, kama kiungo huyo akionyesha
kiwango kikubwa msimu ujao, basi watamuongezea mkataba mwingine.
“Kocha ndiye aliyependekeza Uhuru tumbakize,
hivyo tumeona tumuongezee mkataba mwingine wa mwaka mmoja ambao kama akionyesha
kiwango kizuri, tutamuongezea mwingine.
“Mwanzoni tulishindwa kumpa mkataba kutokana
na Logarusic (Zdravko) kumkataa akidai kuwa haridhishwi na kiwango chake,” kilisema
chanzo hicho.
Uhuru ni miongoni mwa wachezaji wakongwe
waliobaki katika kikosi cha Simba.
0 COMMENTS:
Post a Comment