August 18, 2014

NIYONZIMA (KUSHOTO) AKIWA KWENYE BENCHI LA YANGA. HII ILIKUWA NI MSIMU ULIOPITA.


Kocha Mkuu wa Yanga, Mbrazili, Marcio Maximo, amemuangalia kiungo wake mchezeshaji, Mrwanda, Haruna Niyonzima na kuamua kumtoa kati na kumpeleka pembeni.
Kiungo huyo ana siku tano tangu ajiunge na kikosi hicho kinachofundishwa na Maximo katika kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu Bara.

Mbrazili huyo, katika mazoezi ya hivi karibuni yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Loyola, Mabibo jijini Dar es Salaam, alimpanga Niyonzima kucheza namba saba huku nane akimchezesha Hassani Dilunga.

Maximo alimpanga Niyonzima kucheza nafasi hiyo mara baada ya kupanga vikosi viwili vilivyocheza mechi, kati ya hivyo, kimoja alionekana kuwajaza mastaa wengi kinachodaiwa ndiyo anakiandaa kwa ajili ya kukitumia kwenye msimu ujao.

Wakati mazoezi hayo yanaendelea, kocha huyo alionekana akimpa maelekezo Niyonzima pamoja na beki wa pembeni, Juma Abdul aliyekuwa anacheza namba mbili.

Pia, alionekana kumpa maelekezo kadhaa Dilunga akimtaka kucheza kwenye eneo lake la kati muda wote huku Mbuyu Twite akimsaidia kwenye dimba la kati (namba sita).

Alipoulizwa kocha huyo kuhusiana na sababu za kumbadilisha namba Niyonzima kutoka namba nane hadi saba, alisema: “Katika kikosi changu ninataka kila mchezaji awe na uwezo wa kucheza nafasi mbili hadi tatu na siyo moja pekee.

“Sitaki mchezaji anayeweza kucheza nafasi moja pekee, hiyo itanisaidia siku moja ikitokea mchezaji mmoja amepewa kadi nyekundu au majeruhi, basi mwingine anamrithi.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic