August 25, 2014



mshambuliaji Mario Balotelli ameamua kuchukua jezi kipenzi chake namba 45 ambayo ataitumia akiwa na Liverpool.

Balotelli amekuwa akiitumia namba 45 tokea akiwa Inter Milan, baadaye akajiunga na Man City na hata alipokwenda AC Milan.
Jezi hiyo anaamini ndiyo yenye bahati kwa kuwa wakati akiwa kinda anaichezea Inter Milan, alifunga mabao manne katika mechi nne.
Katika kikosi cha AC Milan, vijana waliochaguliwa kuchezea timu ya wakubwa huvaa jezi kuanzia namba 36 hadi 45.
Kingine Balotelli ambaye leo atashuhudia mechi kati ya Man City dhidi ya timu yake mpya ya Liverpool akiwa jukwaani, amekuwa akitania 4+5=9 akiwa ana maana anavaa jezi namba 9, kijanja.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic