Uongozi wa Yanga umefunguka kuwa upo mbioni
kusaka timu kwa ajili ya mechi ya kimataifa ya kirafiki katika nchi za Afrika
Magharibi, ambapo baadhi ya nchi ni Ivory Coast na Nigeria.
Katibu Mkuu wa Yanga, Beno Njovu, ameliambia
gazeti hili kuwa, wapo katika harakati za kusaka timu ambayo wanaiona itakuwa
na kiwango kizuri ya kuweza kujipima nayo kuelekea msimu wa 2014/15.
“Kocha anahitaji kucheza mechi mbili za
kirafiki za kimataifa kabla ya kuanza kwa ligi, jambo ambalo uongozi
tunalifanyia kazi.
“Tutatafuta
kutoka nchi za Afrika Magharibi, Kusini, Mashariki na Afrika ya Kati, lengo ni
kupata timu bora zitakazotusaidia kuwapima wachezaji wetu vizuri,” alisema
Njovu.
0 COMMENTS:
Post a Comment