September 3, 2014




Na Saleh Ally
DIRISHA la uhamisho kwenye Ligi Kuu England limefungwa usiku wa kuamkia jana huku kukiwa na gumzo kubwa la usajili.

Kati ya usajili uliowavutia wengi uliomalizia dirisha hilo ni ule wa Ramadel Falcao ambaye ametua Manchester United kwa mkopo akitokea AS Monaco ya Ufaransa pamoja na Danny Welbeck kutoka Man United na kujiunga na Arsenal kwa pauni milioni 16.

Mambo yamebadilika kidogo, kama ilivyo hapa nyumbani mara nyingi usajili mkubwa ni Yanga, Simba na Azam FC tu, safari hii karibu kila timu England imefanya usajili na kutumia fedha nyingi, hali ambayo imeshangaza na kuonyesha ushindani kwenye ligi hiyo utakuwa juu zaidi.

Katika fedha za usajili, upande wa manunuzi kwa klabu zote 20 za Premiership, pauni milioni 857.7 zimetumika au euro bilioni 1.09 (zaidi ya Sh trilioni 2.3).

Hiyo ni rekodi mpya kwa kuwa msimu uliopita, pauni milioni 760 na ushee ndizo zilitumika, lakini safari hii tena katika siku mbili za mwisho, imezidi hadi kufikia pauni milioni 850.

Manchester United pekee imetumia pauni milioni 153.1 na kuwa klabu iliyotumia fedha nyingi zaidi katika manunuzi. Huku ikiwa imeuza wachezaji kwa pauni milioni 31.2, maana yake sahihi hasa iliyotumia ni pauni milioni £122.

Timu ambayo imetumia kidogo zaidi ni Stoke City ambayo imetoa pauni milioni 3.4 tu katika usajili ili kupata wachezaji wapya. Pia ikauza kwa fedha chache zaidi kuliko klabu nyingi 19 ambayo ni pauni milioni 3.

Katika klabu hizo 20, zilizoingiza faida ni tatu tu ambazo ni Southampton, Tottehham na Chelsea.

Southampton imeongoza kwa kuingiza faida baada ya kuwauza ghali wachezaji wake watatu ambao ni Adam Lallana, Luke Shaw na Rickie Lambert.

Inayoshangaza zaidi ni Chelsea, ilionekana imetoa zaidi na kuwa moja ya timu imara zaidi katika msimu huu katika mechi za mwanzo lakini bado imeingiza faida.

 Faida:
Timu zilizopata faida ni tatu tu ambazo ni Southampton ambayo imeingiza faida ya pauni milioni 30.7 baada ya kuwa imefanya biashara ya kuuza wachezaji kwa jumla ya pauni milioni 88.5 na kununua kwa pauni 57.9 tu.

Tottenham inafuatia kwa kuwa imeuza wachezaji kwa pauni milioni 40.7 na kununua kwa pauni milioni 34.2 tu, hivyo kufanikiwa kuingiza faida ya pauni milioni 6.5.

Chelsea ndiyo timu ya tatu na ya mwisho katika kuingiza faida katika Premier League kwa kuwa ilinunua wachezaji kwa pauni milioni 87.7 na kuuza kwa pauni milioni 88.5. hivyo faida yake ni pauni 800,000 ambazo zinaingia kibindoni.

Timu nyingine 17 zilizobaki, hakuna hata moja iliyofanikiwa kuingiza faida kwenye Premier League. Maana yake zote zimetoboka mifuko kuhakikisha zinajiimarisha zikihofia msimu huu kuwa utakuwa mgumu maradufu ukilinganisha na uliopita.



TIMU 10 ZILIZOONGOZA KUTOA FEDHA KWA AJILI YA USAJILI (*FEDHA HIZO NI KWA PAUNI MILIONI)


KLABU            IMETOA    IMEINGIZA       IMETUMIA/PATO        GHALI ZAIDI 
Man United       £153.1           £31.2                £122                Angel Di Maria (£59.7) 
Liverpool         £116.8           £81.1                 £35.7               Adam Lallana  (£25.0)
 Chelsea          £87.7             £88.5                £0.8                           Diego Costa (£32.0)
Arsenal               £78.2             £31.8                £46.4                Alexis Sanchez (£35.0)
Southampton    £57.9            £88.6                 £30.7                 Shane Long (£12.0)
Man City            £54.5            £22.5                £32.0               Eliaquim Mangala (£32.0)
Hull City             £39.4            £15.0                £24.4                  Abel Harnandez (£10.0)
Newcastle           £37.8           £12.9                 £24.9                 Remmy Cabella (£12.0)
QPR                    £36.5           £15.5                 £21.0                  Sandro  (£10.0)    
West Ham            £34.5           £3.5                  £31.0              Enner Valencia (£12.0)


Fedha zilizotumika kwa usajili kwa kila msimu tokea 2004:

2004-05      £265 milioni

2005-06       £305 milioni

2006-07       £320 milioni

2007-08       £645 milioni

2008-09       £670 milioni

2009-10       £480 milioni

2010-11       £590 milioni

2011-12       £545 milioni

2012-13       £610 milioni

2013-14       £760 milioni

2014-15       £835 milioni




0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic