September 15, 2014


Kikosi cha JKT Ruvu, kitaanza Ligi Kuu Bara bila ya wachezaji wake saba wa kikosi cha kwanza.

Kocha Mkuu wa JKT Ruvu, Felix Minziro, amethibitisha kutokuwepo kwa wachezaji hao ambao wamekwenda kushiriki michuano ya Majeshi ya Afrika Mashariki iliyokuwa ikifanyika mjini Zanzibar.

“Wachezaji wangu takribani saba wa kikosi cha kwanza, hawapo kwa sasa, hili linanipa wakati mgumu sana, ligi inaanza siku ya Jumamosi, uwepo wao una mchango mkubwa katika timu na wako Msumbiji kwa sasa kulitumikia jeshi katika masuala la michezo.

“Lakini nitaendelea kupambana na msimu ujao tunataka kuonyesha mabadiliko kwa kiasi kikubwa ili kuweza kufanya vizuri na siyo kusuasua kama ilivyokuwa misimu ya nyuma,” alisema Minziro ambaye mara ya mwisho alikuwa kocha msaidizi wa Yanga chini ya kocha Ernie Brandts raia wa Uholanzi.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic