September 23, 2014


Mshambuliaji wa Azam FC, Didier Kavumbagu amesema kikosi chao kitafunga mabao mengi zaidi msimu huu.
Kavumbagu raia wa Burundi, amesema kikosi chao ambacho safu yake ya ushambuliaji, kiungo na walinza wana ushirikiano mkubwa, watafunga mabao mengi zaidi.

Akizungumza baada ya mechi dhidi ya Polisi, Kavumbagu alisema Azam FC ina ushirikiano wa juu, hali inayotoa nafasi karibu kila mchezaji kuwa na nafasi ya kufunga au kutoa pasi za mabao.
“Mimi ninaamini tutafunga mabao mengi zaidi. Washambuliaji tunaelewana vizuri na viungo.
“Bado utaona kwa Azam hata mabeki wanaweza kufunga, subiri ligi inaendelea utakubali ninachosema,” alisema Kavumbagu.

Mrundi huyo aliyekipiga Yanga msimu uliopita ameanza ligi kwa kupachika mabao mawili katika ushindi wa 3-1 dhidi ya Polisi Moro iliyopanda daraja.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic