September 23, 2014

PHIRI AKIWA MAZOEZINI ZANZIBAR.

Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Phiri amesisitiza wachezaji kusahau kuhusiana na mechi waliyotoka sare ya mabao 2-2 dhidi ya Coastal Union.

Phiri ametaka wachezaji wake kujifunza kupitia mchezo huo na wayarekebishe wakati watakapokutana na Polisi Moro, Jumamosi.
“Kukumbuka makosa ni jambo zuri kwa ajili ya kurekebisha, kila siku zinavyokwenda unatakiwa kupunguza kiwango cha kusahau.
“Halafu unaweka nguvu nyingi kwenye mafunzo kwa ajili ya kurekebisha kosa ulilofanya.
“Tuikuwa na mengi tuliyokosea, sawa walinzi walifanya uzembe, lakini washambuliaji pia walipoteza nafasi muhimu.
“Kuna wakati viungo pia walikosea jambo nah ii ndiyo maana ya timu,” alisema Phiri na kuongeza.
“Sasa ni wakati wa kujirekebisha na siku ya mechi ijayo, tufanye kazi bora zaidi.”
Simba iko Zanzibar imeanza kazi kwa ajili ya kujiwinda kuwavaa Polisi Moro ambayo itakuwa ni mechi yake ya pili.

Katika mechi dhidi ya Coastal, Simba ilitangulia kwa mabao 2-0 hadi mapumziko, kipindi cha pili, Coastal ikarudisha yote na kuwapa presha kubwa ikikaribia kufunga la tatu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic