September 19, 2014


Kitendo cha kubadilishana jezi kilichofanywa na viungo washambuliaji, Mrisho Ngassa wa Yanga na Salum Abubakar ‘Sure Boy’ wa Azam FC, katika mechi ya Ngao ya Jamii, kilikuwa ni danganya toto kwa mashabiki waliohudhuria mchezo huo.


Mashabiki waliokuwepo uwanjani hapo, waliwashuhudia viungo hao wakibadilishana jezi wakati wa mapumziko walipokuwa wakielekea vyumbani, kitendo ambacho kilipongezwa na wengi kuwa ni uungwana.

Timu hizo zilikutana Jumapili iliyopita kwenye Uwanja wa Taifa katika mechi ya Ngao ya Jamii ambapo Yanga ilishinda kwa mabao 3-0.

Ofisa Habari wa Azam, Jaffari Iddi alipoulizwa juu ya kitendo hicho alifunguka kwa kusema: “Tukio hilo lilifanyika kwa ajili ya kuonyesha michezo ni upendo lakini kila mmoja alichukua jezi yake walipofika katika vyumba vyao vya kubadilishia nguo. Lilikuwa tukio zuri la kuonyesha uungwana na upendo baina ya timu hizo.”

Kitendo cha wachezaji hao kubadilishana jezi wakati wa mapumziko kiliwashitua mashabiki wengi wa soka.
Huenda walianza kuhisi kuwa tukio kama lile la misimu miwili iliyopita wakati Ngassa akiwa Azam FC halafu akachukua na kuibusu jezi ya Yanga, litajitokeza tena.

 


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic