September 20, 2014


Na Saleh Ally
KWA miaka kumi sasa tokea 2004, inaonekana kumekuwa na mchuano mkali sana katika suala la ufungaji mabao kwenye Ligi Kuu Bara.

Awali ilionekana kama washambuliaji kutoka nyumbani wamelala kwa kuwa wageni wanatawala zaidi kila unapofika mwisho wa msimu na hesabu kupigwa nani ni mfungaji bora.

Tokea mwaka 2004 ni misimu kumi, wenyeji wamekuwa wafungaji bora mara tano, sambamba na wageni.
Maana ya yake msimu huu mpya, itakuwa ni fainali, kuwa katika kipindi cha miaka 11, iwapo atashinda mwenyeji, watakuwa wamewashinda wageni au wakishinda wao, wenyeji watakuwa wameangushwa.
Bado wenyeji wanashikilia rekodi ya mabao mengi zaidi, msimu wa 2006-07, Abdallah Juma aliyekuwa anakipiga Mtibwa Sugar, alipiga mabao 40. Hakuna mgeni wala mwenyeji aliyefikia idadi hiyo.
Boniface Ambani (Yanga), John Bocco (Azam FC) na Amissi Tambwe wa Simba, msimu uliopita ndiyo walijaribu kumkaribia baada ya kufikisha mabao 19.
Bado wachezaji wenyeji wana changamoto kubwa kwa kuwa kwa misimu miwili sasa wafungaji bora wa Ligi Kuu Bara wametokea nje, Kipre Tchetche-Ivory Coast na Tambwe-Burundi.
Watakubali wageniw apige ‘hat-trick’ ya ufungaji bora, au mmoja atakataa na kuibuka na nafasi hiyo?
Inawezekana lakini haitakuwa kazi lahisi, angalia Simba ina watu kama Paul Modo Kiongera, Emmanuel Okwi na Tambwe.
Cheki Yanga ina mambo mapya, Wabrazil wawili, Jaja na Coutinho ambao wameanza kuonyesha wana kitu fulani. Hivyo haitakuwa kazi lahisi na ushindani wao utavuta mengi.
Washambuliaji na viungo wa kigeni wamekuwa wakitaka kuonyesha umuhimu wao kuwa fedha nyingi kutumia dola ambazo wamekuwa wakilipwa, wanastahili.
Lakini wanasaidia kuleta changamoto kubwa kwa wenyeji ambao wanataka kuonyesha kinachofanywa na wageni wala si ishu, wao pia wako fiti.
Ligi Kuu Bara inaanza rasmi leo, viwanja vitawaka moto kila timu ikitaka kuanza na mguu bora wa kwanza.


WAFUNGAJI BORA TANGU 2004:
Mwaka     Nchi            Mfungaji                Timu        Mabao
2004/05  Tanzania     Abubakar Mkangwa   Mtibwa     16
2005/06  Somalia     Cisse Abshir           Simba      19
2006/07  Tanzania   Abadallah Juma       Mtibwa       20
2007/08  Uganda    Mike Katende   Kagera        11
2008/09  Kenya Boniface Ambani  Yanga        18
2009/10  Tanzania Mussa Mgosi Simba        18
2010/11  Tanzania Mrisho Ngassa  Azam        18
2011/12  Tanzania  John Bocco         Azam       19
2012/13    Ivory Coast   Kipre Tchetche      Azam       17
2013/14    Burundi       Amissi Tambwe     Simba        19



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic