September 22, 2014


Baada ya kuiongoza timu yake kupata ushindi mnono wa mabao 2-0 dhidi ya Yanga huku Mbrazili mmoja, Geilson Santos ‘Jaja’ akiwemo dimbani, Kocha Mkuu wa Mtibwa Sugar, Mecky Maxime, amewaponda Wabrazili wa Yanga akisema ni wachezaji wa Uwanja wa Taifa tu.


Mtibwa iliendeleza ubabe wake kwa Yanga kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro, juzi mbele ya mashabiki kibao waliojitokeza, shukrani kwa mabao ya mkongwe Mussa Mgosi na Ame Ali.


Lakini baada ya mchezo huo, Maxime ambaye alimfunga kocha wake wa zamani wa Taifa Stars, Marcio Maxime, alisema Jaja na Coutinho watapata tabu sana watakapokuwa wakicheza kwenye viwanja vya mikoani kutokana na kuwa vibovu.

Alisema katika mechi yao, Jaja alipata wakati mgumu sana kucheza kutokana na uwanja kuwa mbovu lakini kama angekuwa akicheza kwenye Uwanja wa Taifa, pengine angefanya maajabu kama ilivyokuwa dhidi ya Azam katika mchezo wa Ngao ya Jamii.

Jaja alikosa penalti ambayo ingeweza kuipatia Mtibwa bao la kusawazisha.
“Jaja siyo mbaya ni mchezaji mzuri sana ila viwanja vya Tanzania vitamsumbua sana, mpaka aje kukaa sawa itamchukua muda mrefu.
“Kwa jinsi ninavyoona mchezaji huyo na mwezake watakuwa wakifanya vizuri tu watakapokuwa kwenye Uwanja wa Taifa kwa sababu ni mzuri ukilinganisha na hivi vya mikoani, ambavyo wachezaji wetu wamevizoea,” alisema Maxime.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic