Ndanda FC imeonyesha imepania kufanya kweli, imeichapa Stand
United kwa mabao 4-1.
Ikiwa ndiyo mechi ya kwanza kwa timu hizo ya Ligi Kuu Bara, Stand
ikiwa nyumbani Kambarage imelala kwa mabao hayo 4-1.
Wageni Ndanda walipata mabao yao kupitia Paul Ngalema, Nassor
Kapama na Ernest Mwalupani.
Wakati wenyeji ambao walijitahidi kurekebisha mambo walipata bao
la kufutia machozi kupitia kwa Salum Kamana.
Mechi ilikuwa nzuri nay a kuvutia lakini wageni ndiyo walioonyesha
soka la kuvutia zaidi.
0 COMMENTS:
Post a Comment