Na Saleh Ally
KWA watu wa Afrika
Mashariki, Southampton ya England ni moja ya timu maarufu sana kutokana na
jambo moja.
Mkenya, Victor Wanyama
anakipiga katika kikosi hicho. Hivyo wengi wamekuwa wakipenda kukifuatilia kila
kinapokuwa inacheza.
Kwenye vitongoji mbalimbali
vya jiji la Nairobi, timu hiyo imekuwa ikijikusanyia mashabiki kwa haraka sana
na hata kufikia kuonekana ni biashara kwa wale ambao hufanya biashara ya
kuonyesha mpira.
Lakini kwa sasa Southampton
imekuwa maarufu zaidi duniani kote. Si timu ya siku hizi, lakini msimu uliopita
imezua gumzo baada ya kuuza wachezaji watano wa kikosi cha kwanza.
Southampton imeuza wachezaji wake watano wa kikosi cha kwanza
kwenye timu za Liverpool, Manchester United na Arsenal. Kitendo hicho kilizua
hofu kubwa mashabiki wake wakiamini watakuwa wamejivuruga.
Southampton imekuwa moja ya
klabu zilizoingiza kiasi kikubwa cha fedha kutokana na mauzo ya wachezaji,
imepata pauni milioni 97, hiki ndicho wanachotaka viongozi.
Hapa nyumbani kabisa linalosifika
kwa mipango ya biashara ni Wachaga. Unaweza ukawaita Southampton ni Wachaga wa
England kutokana na walichokifanya msimu uliopita.
Wamekuwa gumzo dunia nzima
kutokana na kuwaza beki Luke Shaw aliyetua Man United kwa (£30million) na Calum Chambers (£16milioni)
aliyejiunga Arsenal.
Adam Lallana (£25milioni),
Rickie Lambert (£4milioni) na Dejan Lovren (£20milioni), wote wamejiunga na Liverpool.
Mashabiki walionekana
kupania, kwamba timu imeuza nyota kadhaa wakiwemo watano wa kikosi cha kwanza,
hivyo wakaingia hofu. Wako walijipanga kusema uongozi umekosea kwa ajili ya
kuusema.
Lakini baada ya kuanza kwa
Ligi England, katika mechi nne walizocheza wamekuwa na wastani mzuri hata
kuliko baadhi ya timu walizoziuzia wachezaji.
Walianza na kipigo cha
mabao 2-1 dhidi ya Liverpool wakiwa ugenini, baada ya hapo wakapata sare ya
bila mabao dhidi Wes Brom, wakiwa nyumba na kelele zikaanza.
Wakatoka nje ya kuwatwanga
West Ham 3-1, halafu wakarejea nyumbani na kushinda kwa mabao 4-0 dhidi ya
Newcastle.
Kelele zimezimika, huenda
wako wanaosubiri kulaumu lakini ukweli uongozi wa Southampton umeonyesha kile
kilichoonekana hakiwezekani. Kwanza timu isiyo na jina kubwa kama Man United au
Arsenal. Imetengeneza wachezaji, ikawategemea na kuwauza.
Halafu baada ya hapo
imeendelea kufanya vizuri. Maana yake imefanya biashara na kuendelea kufanya
vizuri kisoka.
Huo ndiyo uongozi sahihi,
huenda hata hapa nyumbani viongozi wanapaswa kujifunza wao kuongoza na
kuonyesha mifano ambayo haijategemewa, badala wao kufanya wanavyotaka mashabiki
au wanachama.
Siku zote wanachama
wanataka kuburudika tu, viongozi wanataka fedha ili kuendesha klabu kwa
mafanikio.
Mapinduzi hutengenezwa na
viongozi imara kama wale wa Southampton ambao hata kama timu yao haitafanya
vizuri sana, bado wao ni mashujaa kwa kuwa walisimamia wanachokiamini na
kimefanya kazi.
Nyumbani Tanzania kunaweza
kuwa mfano au sehemu nzuri ya kujifunza hilo hasa kwa viongozi wengi wa Yanga
na Simba hufanya maamuzi kuwafurahisha tu mashabiki.
Mabadiliko mara nyingi
hayaanzi kwa kufurahisha kama walivyofanya Southampton. Lakini watu waumie na
wanaoamua kuyaanzisha lazima wawe jasiri kama walivyofanya viongozi hao wa
Southampton.
TIMU ZILIZOONGOZA KWA KUUZA WACHEZAJI:
1. Southampton FC £97m
2. Real Madrid CF £89.4m
3. Chelsea FC £81m
4. Liverpool FC £80m
5. AS Monaco £76m
6. FC Barcelona £68.7m
7. FC Porto £67m
8. Atlético Madrid £58.2m
9. Sevilla FC £43m
10. Bayern Munich £39m
11. Real Sociedad £36.7m
11. Real Sociedad £36.7m
12. AS Roma £36.7m
13. Benfica £34.3m
14. Valencia C£32.7m
15. Udinese £31
16. Tottenham £30.3m
17. Athletic Bilbao £28.7m
18. Man United £27m
19. Hellas Verona £23m
20. Cardiff City £22.3m
MECHI ZA EPL ILIZOCHEZA:
Liverpool
2-1Southampton
Southampton
0-0 Wes Brom
West
Ham 1-3 Southampton
Southampton
4-0 Newcastle
0 COMMENTS:
Post a Comment