PAMOJA na historia zinazogongana lakini
ukweli kabla ya jina la Simba, kulikuwa na majina kadhaa yalipita wakati wa
uasisi wa klabu hiyo.
Kweli klabu hiyo ilizaliwa mwaka 1936 baada
ya kujitenga kutoka kwa New Youngs ambayo sasa ni Dar Young African au Yanga kutokana
na watu hao waliokuwa timu moja kupingana baada ya kutoridhishwa na uendeshwaji
wake.
Waliojitenga ambao wengi walikuwa ni wasomi
ambao walisisitiza wakitaka mambo yao kuendeshwa kisomi waliunga timu inayoitwa
Eagle Night na katika miaka ya 1940 wakaibadlisha na kuibandika jina la
Sunderland.
Hapo ndiyo chimbuko la kuvaa jezi za rangi
nyekundu kama ilivyo Sunderland ya England lilishika kasi lakini mwaka 1971,
jina Simba likazaliwa rasmi.
Pamoja na hivyo kumekuwa na taarifa kwamba
Simba imewahi kuitwa Queens Sports Club, lakini bado wengi wamekuwa wakipinga
kwamba hakukuwahi kuwa na jina hilo au lilipendekezwa na halikuwa kutumika
zaidi ya lile la Stanley katika kipindi hicho.
Waliojiondoa New Youngs na kuunda timu mpya
ni baada ya kufanya vibaya kwenye Ligi Daraja la Kwanza Tanganyika mwaka 1936
baada ya kushinda mechi tatu tu kwenye ligi hiyo na kuishia kushika mkia baada
ya mechi 12.
Mzozo ulitokana na upangaji wa timu na kwa
sababu New Youngs ilikuwa ndiyo imepanda daraja kwa kufanya vizuri sana daraja
la pili, baadhi ya waliojiengua waliona hakukuwa na umakini pia katika suala la
kujali gharana kama ile ya Sh 15 ya ada ya ushiriki wa ligi.
Bado waliona gharama zilikuwa nyingi, mfano
zilizotumika kununua vifaa kwa ajili ya wachezaji na ushonaji wa jezi. Kikubwa
kwao waliona mambo hayaendi kisomi, au kimpangilio, hivyo wakaunda timu mpya na
ndiyo mwanzo wa kuzaliwa na Simba ambao wamekuwa wakiita ni wataratibu, waelewa
na wanaopenda soka la kutandaza badala ya lile la haraka na kukurupuka.
Jina Stanley lilikuwa ni la Mtendaji Mkuu wa
Serikali ya Uingereza ambao walikuwa watawala wa Tanganyika wakati huo. Jina la
mkoloni huyo lilikuwa pia ni la moja ya barabara za mitaa ya Dar es Salaam
ambako yalikuwepo makao makuu ya klabu hiyo ilipoanza.
Kwa sasa barabara ya Staley inajulikana kama
barabara ya Aggrey ambayo ni moja ya mitaa maarufu sana jijini Dar es Salaam.
Lakini sababu nyingine zilizoelezwa
kujitenga kwa vijana hao waliamini ulikuwa ni wakati mwafaka wa kuongeza timu
nyingi za Waafrika au wenyeji ili waweze kupambana na timu za Waasia na Wazungu
ambazo ndiyo zilionekana kufanya vizuri huku zile chache za wenyeji zikipanda
na kushuka daraja kila kukicha wakati wa ligi iliyokuwa ikiendeshwa kwenye
Viwanja vya Gymkhana.







Nice report
ReplyDelete