September 2, 2014


Thika United imetua jijini Dar tayari kwa mechi yake ya kesho dhidi ya Yanga ambayo itakuwa ni ya kwanza ya kirafiki ya kimataifa ya Marcio Maximo.

Mbali na hivyo, mechi hiyo itakuwa ni ya kwanza ya Maximo akiwa na Yanga kwenye Uwanja wa Taifa.
Pia itakuwa ya kwanza ya Maximo katika ardhi ya Tanzania Bara baada ya kuingoza Yanga katika mechi za kirafiki, zote zikiwa zimepigwa visiwani Zanzibar.
Thika kutoka Kenya itakipiga na Yanga katika mechi ya kirafiki ya kimataifa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.
George Otieno ambaye ni mmoja wa maofisa wa Thika amesema lengo lao ni kuta kuifunga tu Yanga.
“Sisi tuko vizuri na tunachotaka ni ushindi, hatuwezi kufunga safari kutoka Kenya kuja kushindwa.

“Tunajua Yanga ni timu kongwe kuliko sisi, bora kwa maana ya ukongwe lakini kiwango chetu kipo juu zaidi,” alisema.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic