October 6, 2014


LIVERPOOL, England
PAMOJA na kuwa katika wakati mgumu akionekana hafungi licha ya kwamba amenunuliwa kwa kitita cha pauni milioni 16 (Sh bilioni 37) kutoka AC Milan, mshambuliaji Mario Balotelli ndiye anaongoza kwa wastani mzuri wa mashuti langoni.


Soka lina misemo yake na unapozungumzia wapiga mashuti basi wenyewe wanawaita wapiga mawe.

Balotelli tayari ana wastani wa mashuti mengi anayopiga na kulenga lango kuliko mchezaji mwingine wa Ligi Kuu England.

Balotelli ana wastani wa mashuti matano katika kila mchezo aliocheza ambayo amepiga na kulenga lango.

Hii inaonyesha wakati wowote anaweza kurejea kwenye listi ya wachezaji wanaofunga kwa kuwa mashuti yake yanalenga lango zaidi.

Wanaomfuatia ni Graziano Pelle wa Southampton, Sergio Aguero (Man City) na Diego Costa wa Chelsea ambao kila mmoja ana wastani wa mashuti manne kwa mechi.

Hapa kuna kitu kinaonyesha kuwa Balotelli yuko kwenye kundi la washambuliaji hatari kwa maana ya kupiga mashuti, lakini ameshindwa kuwa mjuzi zaidi na kufunga.

Washambuliaji wenye wastani wa mashuti manne kila mmoja ambao wako chini yake kiwastani kwa mashuti, ndiyo wanaosumbua kwa ufungaji mabao.

Costa ndiye anaongoza ufungaji bora akiwa na mabao kumi (kabla ya mechi ya jana), Aguero ana matano na Pelle amepachika manne.

Hivyo ni kazi kwake kurekebisha mambo na kufanya aingie kwenye listi ya wapachika mabao na si wapiga mashuti yanayolenga tu.

Kwa upande wa timu, Chelsea wamefunga mabao 19 kabla ya mechi ya jana dhidi ya Arsenal wakifuatiwa na Man City wenye 14.

Wao pia ndiyo wanaongoza kwa wastani wa kupiga mashuti mengi yaliyolenga lango wakiwa na 18 kwa mechi moja.

Man City wanawakimbiza kwa karibu wakiwa na wastani wa mashuti 17 kwa mechi moja, halafu Liverpool wenye 16 na Arsenal wana 15.

Hii ni mapema sana kwenye ligi hiyo, lakini kila baada ya mechi moja au mbili kunakuwa na mabadiliko kwa kuwa wachezaji wanang’amua kipya cha kufanya, hali kadhalika makocha.



 Mashuti kwa mechi:

Chelsea       18

Man City       17

Liverpool       16

Arsenal       15

Newcastle       14



Mashuti kwa mechi:

Mario Balotelli - Liverpool         5

Graziano Pellè - Southampton       4

Sergio Agüero-Man City       4

Diego Costa       -Chelsea       4

Charie Austin-QPR       3



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic