October 6, 2014


Mashabiki wa Simba walioonekana na machungu, walimvaa mshambuliaji Mganda wa timu hiyo, Emmanuel Okwi, huku wakimhoji kwa nini timu haifanyi vizuri, juzi.


Lakini shabiki mmoja, yeye alienda mbali, kwani alijitokeza mbele akitaka kumfanyia fujo, jambo ambalo lilizua fujo na polisi kulazimika kuingilia kati na kuwatawanya mashabiki hao. Ilikuwa ni baada ya mechi dhidi ya Stand United kwenye Uwanja wa Taifa, Simba ilimaliza mechi hiyo kwa sare ya bao 1-1- ikiwa ni tatu mfululizo msimu huu.

Juzi, tafrani ilikuwa kubwa kwenye basi la Simba, mashabiki walilizingira na kuanza kuwatolea maneno makali wachezaji, wakilalamika kwa nini wanashindwa kufanya vizuri.

Lakini Okwi ndiye aliyeonekana kuzongwa zaidi na mashabiki hao waliokuwa wamepandwa na jazba.

Kama siyo polisi waliokuwa karibu na eneo hilo kuingilia kati, pengine hali ingekuwa mbaya zaidi.


Okwi bado hajafanya kile kilichotarajiwa na mashabiki wa Simba, baada ya kutua msimu huu kwa usajili uliozua utata akitokea Yanga ambayo ilikuwa na mgogoro naye.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic