October 20, 2014


Si unajua wachezaji wanapenda kushangilia kwa sarakasi kama ilivyokuwa kwa Luis Nani aliyekuwa Man United, sasa yuko Sporting Lisbon ya Ureno. Sasa watambue hiyo ni hatari.

Mchezaji mmoja wa India amefariki dunia wakati akijaribu kushangilia baada ya kufunga bao kwenye Ligi Kuu Soka nchini India.

Peter Biaksangzuala amefariki dunia jana Jumapili wakati akitibiwa hospitalini.
Mara baada ya kuifungia timu yake ya Bethlehem Vengthlang FC alikimbia kwenda kushangilia na kujaribu kuruka ‘samasoti’, akaanguka vibaya na kuvunja uti wa mgongo.

Kijana huyo aliyekuwa na umri wa miaka 23 alifunga bao la kusawazisha katika dakika ya 62 dhidi ya Chanmari West FC.
Kocha wa zamani wa Man United, Alex Ferguson aliwahi kumzuia Luis Nani kuruka sarakasi wakati wa kushangilia bao.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic