October 14, 2014


Katibu Mkuu wa zamani wa Simba, Kassim Dewji amewataka mashabiki wa Msimbazi kutotegemea mambo makubwa sana katika mechi yao ya Oktoba 18 dhidi ya Yanga.

Dewji ambaye yuko Johannesburg, Afrika Kusini ambako kikosi cha Simba kimeweka kambi, amesema bado kuna mambo mengi yanapaswa kubadilishwa.
“Kikosi hiki kina mambo mengi ambayo unayaona kadiri siku zinavyokwenda, uongozi unafanya juhudi, benchi la ufundi linajituma.
“Unajua, kunamabadiliko yanafanyika na kawaida kwenye mabadiliko kunahitaji muda, haiwezi kuwa mara moja tu kila kitu kinabadilika.
“Mechi inayokuja dhidi ya Yanga, mashabiki wasitarajie makubwa sana kutokana na hali hii,” alisema Dewji.
“Lakini haina maana timu itaingia uwanjani kwenda kufungwa, tutapambana kwa kuwa ndiyo utamaduni wa Simba, kupambana na kuwapa heshima mashabiki na wanachama.
“Ndiyo maana nasisitiza kutotegemea makubwa sana, watu waamini timu bado inabadilishwa, inapita kipindi kigumu cha mpito kutoka katika kipindi ambacho Simba iliporomoka, hivyo tuwe wavumilivu kidogo, tuuamini uongozi, tuwaamini watu wa benchi la ufundi.”

Simba inatarajia kucheza mechi yake ya kirafiki kesho dhidi ya Jomo Cosmos.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic