October 20, 2014


Kipa wa Yanga, Deogratius Munishi ‘Dida’ amesema kipa kinda wa Simba, Peter Manyika, ndiye anastahili kuwa mchezaji bora wa mechi yao ya Jumamosi.

Dida alifunguka kuwa kama angepewa nafasi ya kuchagua mchezaji bora wa mechi katika mchezo wa juzi kati ya Yanga na Simba, bila kipingamizi angempa tuzo yosso huyo wa miaka 18, kauli iliyoungwa mkono na kipa mkongwe nchini, Juma Kaseja.
DIDA

Manyika ambaye ni mtoto wa kipa wa zamani wa Yanga na Taifa Stars, Manyika Peter, alikuwa gumzo uwanjani hapo kwa kiwango kizuri alichoonyesha huku akichomoa michomo mikali, ukiwemo wa Andrey Coutinho ambaye walikuwa uso kwa uso langoni.
KASEJA
“Lazima tuseme ukweli Manyika amefanya kazi kubwa ambayo hakuna aliyeitarajia katika mchezo mkubwa kama huu, hata mimi sikutarajia kama angeweza kufanya vile na ninaweza kusema kuwa alikuwa ‘man of the match’ kwa ukweli ulio wazi,” alisema.
Wakati huohuo, Kocha wa Simba, Patrick Phiri, amekiri kwamba Manyika ndiye aliyekuwa mchezaji bora kwenye mechi hiyo ya watani juzi.

“Kwa upande wangu Manyika ndiye mchezaji bora katika mechi ya leo (juzi), ukiangalia ameokoa mipira mingi yeye akiwa na washambuliaji wa Yanga ndani ya 18.
“Isitoshe mechi hii ni ya kwanza kwake kwenye ligi kuu tukiwa tunakutana na Yanga, ninampongeza sana Manyika amecheza vizuri sana,” alisema Phiri.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic