October 20, 2014

MANJI
Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji amelishauri Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuiangalia adhabu ya kumfungia miaka saba mwanasheria Dk Damas Daniel Ndumbaro asijihusishe na masuala ya soka.

Manji ameiambia TFF wakati ilipokutana na viongozi wa juu wa klabu za Ligi Kuu Bara, juzi kabla ya Yanga na Simba hazijavaana.
Habari za uhakika kutoka ndani ya kikao hicho zimeeleza, Manji alimshauri Malinzi kuiangalia adhabu hiyo ya Dk Ndumbaro kwa kuwa kujenga familia ya soka si kufungiana.
DK NDUMBARO

“Manji amewaambia TFF kwamba hakuna sababu ya kufungiana, kama kuna hali ya kutoelewana, iko haja ya kujadiliana na kufikia mwafaka,” kilieleza chanzo.
“Manji alisema hayo wakati akichangia mambo kadhaa, hata hivyo mkutano haukuwa mrefu sana, watu wakakimbilia mpirani,” kilisisitiza chanzo.
Dk Ndumbaro ambaye ni daktari wa sheria yuko nchini Marekani kwa mwaliko wa moja ya vyuo vikuu nchini humo, alifungiwa baada ya kuzitetea klabu zisikatwe asilimia tano kutoka kwenye fedha za wadhamini.

Wakati anafungiwa, Dk Ndumbaro ambaye hakusikilizwa, alikuwa tayari ameondoka nchini kwenda Marekani.

1 COMMENTS:

  1. Huyo Ndumbaro hana tofauti na Dr.Majimarefu wa Simba tuu!

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic