October 7, 2014


SEIF MAGARI AKIWA NA MWANAYE KATIKA MOJA YA MECHI ZA YANGA.
Kocha Marcio Maximo wa Yanga, kesho atakutana na sehemu ya uongozi wa Yanga kueleza mikakati yake.

Mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Yanga, Seif Ahmed ‘Magari’ amesema wanakutana na Maximo ili kujadili maandalizi yao kwa ajili ya mechi ijayo dhidi ya Simba Oktoba 18.
Magari amesema baada ya kukutana na Maximo na wasaidizi wake, watamsikiliza na baadaye kujadiliana.
“Mwalimu ndiye anayejua maandalizi yanavyotakiwa kuwa, lakini tutamsikiliza na kushauriana.
“Tunajua mechi dhidi ya Simba itakuwa ngumu, tunachotaka ni pointi tatu lakini muhimu ni kutambua ugumu wa mechi.
“Pia tunajua mechi itakuwa ngumu, lakini tutapambana kuhakikisha tunafanya vizuri,” alisema Magari.
Mechi hiyo ya watani, tayari imekuwa gumzo na mashabiki wanaisubiri kwa hamu kubwa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic