Na Saleh Ally
KASI ya wapachika mabao England inazidi kupamba moto, tumekuwa
tukijaribu kuifuatilia kwa kasi kubwa.
Washambuliaji wa timu 20 za England wanachuana vikali, kila mmoja
akitaka kuchukua nafasi ya ufungaji bora wa ligi hiyo.
Si kazi rahisi, ukweli uko hivi, kama ni taji sasa halina mwenyewe
kwani mfungaji wa msimu uliopita, Luis Suarez aliyekwamisha mipira 31 wavuni,
sasa yuko Hispania akikipiga katika kikosi cha Barcelona.
Nani atakuwa mfungaji bora? Hilo ni swali la kwanza lakini yupi
ataonyesha uwezo mkubwa wa upachikaji mabao kwa kasi na uwezo wa aina yake? Nani
ana kitu au vitu vya ziada katika kazi hiyo.
Ufungaji ni kipaji, mafunzo yanaweza kuongeza uwezo zaidi au utamu
wakati mfungaji anausindikiza mpira wavuni kumaliza kazi yake ya hesabu ya
mabao.
Kufunga mara nyingi ni sehemu tatu kuu, nyingine zinaweza kufuatia
kwa ziada. Moja, mguu wa kulia, pili wa kushoto na tatu ni kichwa. Vingine,
kama kifua, tumbo au vinginevyo vinaweza kutokea bila ya kutarajiwa.
Diego Costa wa Chelsea, amezidi kuonyesha kasi ya aina yake baada
ya kupachika bao lake la tisa katika mechi ya saba, lakini wapo wanaoonekana
hawako mbali naye kama Sergio Aguero mwenye mabao 6 na Leonardo Ulloa na
Berahino wenye matano.
Idadi ni kitu muhimu kabisa kwa kuwa ndiyo kinachofunga mahesabu,
lakini nani mwenye uwezo mkubwa wa kutumia silaha zote tatu, lakini yupi ana
uwezo wa kufunga ndani na nje ya 18?
Costa amefunga mabao yake yote ndani ya 18, lakini matatu mguu wa
kulia, manne kushoto na mawili ameyashindilia kwa kichwa, hali inayoonyesha ni
hatari sana.
Aguero amefunga mabao yote sita kwa mguu wa kulia, tofauti yake na
Costa ni kuwa, manne amefunga ndani ya 18 na mawili akiwa nje ya eneo hilo.
Ulloa ambaye anatikisa pia ambaye ana mabao matano, mawili kafunga
na mguu wa kulia, moja kushoto na mawili kwa kichwa, kama ilivyo kwa Costa,
yote amekwamisha akiwa ndani ya 18.
Wafungaji hawa ukiwafuatilia utagundua kuna burudani ya aina yake
kwa kuwa kila mmoja ana ujuzi wa aina yake, unaotofautiana na mwenzake na
kusababisha ushindani baina yao kuwa mkali na mwisho hujui nani atamaliza akiwa
mfalme wa kutikisa nyavu England. Angalia takwimu.
MECHI DAKIKA
MGUU KULIA KUSHOTO KICHWA NDANI YA 18
NJE MABAO
Diego Costa 7 585
3
4 2
9 0
9
Sergio Aguero 8 532 6
0 0
4 2 6
Leonardo Ulloa 7 568 2
1 2
5 0
5
Berahino 7
628 4 0 1
5 0 5
Naishmith 7
567
2 1 1
4 0 4
Pelle 7 630 2 1 1
4 0 4








0 COMMENTS:
Post a Comment